Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  Uganda General Claims Ability to Seize Tehran in 14 Days, Draws Global Skepticism

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  Unpopular Opinion: Noah Lyle Is Still Steps Ahead Of Letsile

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    Football Titbits Across The Papers

    Manchester United and Tottenham have made moves to sign Netherlands forward Crysencio Summerville, 24, from West Ham. (Teamtalk), external Chelsea are monitoring 26-year-old Porto goalkeeper Diogo Costa as they consider…

    Read more

    The World Cup Drama Continues! Round 2 Starts Today

    The World Cup drama continues! Round 2 starts today. 7pm | Czech Republic 🇨🇿 vs South Africa 🇿🇦 10pm | Switzerland 🇨🇭 vs Bosnia 🇧🇦 1am | Canada 🇨🇦 vs…

    Read more

    You Missed

    Football Titbits Across The Papers

    • By Milton
    • June 18, 2026
    • 2 views
    Football Titbits Across The Papers

    The World Cup Drama Continues! Round 2 Starts Today

    • By Milton
    • June 18, 2026
    • 3 views
    The World Cup Drama Continues! Round 2 Starts Today

    Update: Cole Palmer’s Connection With Chelsea’s Attack Was Reflected In The Chances He Created For Those Around Him

    • By Milton
    • June 3, 2026
    • 10 views
    Update: Cole Palmer’s Connection With Chelsea’s Attack Was Reflected In The Chances He Created For Those Around Him

    𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆: These Are The 𝐂𝐎𝐍𝐅𝐈𝐑𝐌𝐄𝐃 𝐍𝐄𝐖 𝐑𝐔𝐋𝐄𝐒 For The 2026 World Cup

    • By Milton
    • June 3, 2026
    • 17 views
    𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆: These Are The 𝐂𝐎𝐍𝐅𝐈𝐑𝐌𝐄𝐃 𝐍𝐄𝐖 𝐑𝐔𝐋𝐄𝐒 For The 2026 World Cup

    Update: Gachagua’s Team Unites For Upcoming Ol Kalou parliamentary By-election

    • By Milton
    • June 3, 2026
    • 12 views
    Update: Gachagua’s Team Unites For Upcoming Ol Kalou parliamentary By-election

    𝗔𝗡𝗔𝗟𝗬𝗦𝗜𝗦: Pentagon Targets 300,000 Kamikaze Drones In Major Military Expansion

    • By Milton
    • June 3, 2026
    • 17 views
    𝗔𝗡𝗔𝗟𝗬𝗦𝗜𝗦: Pentagon Targets 300,000 Kamikaze Drones In Major Military Expansion