Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  BREAKING: Former SSFF President Augustino Maduot Airlifted To Nairobi After Suspected Food Poisoning In Juba

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  Rais Wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan Awaachia Waandamanaji Huru

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    What Has Your Area Governor Done?

    In just three years, the Kiambu County Governor has overseen the construction of six new Level Four hospitals and 26 Level Three hospitals across the county. These facilities are already…

    Read more

    • MiltonMilton
    • News
    • January 11, 2026
    • 13 views
    • 5 minutes Read
    Are You Struggling with Family Disputes? Here’s What Can Bring Peace and Unity

    Family is meant to be a source of love, support, and comfort, but for some, it can be a battleground. Conflicts, misunderstandings, and old grudges can create a toxic atmosphere,…

    Read more

    You Missed

    What Has Your Area Governor Done?

    • By Milton
    • January 11, 2026
    • 8 views
    What Has Your Area Governor Done?

    Are You Struggling with Family Disputes? Here’s What Can Bring Peace and Unity

    • By Milton
    • January 11, 2026
    • 13 views
    Are You Struggling with Family Disputes? Here’s What Can Bring Peace and Unity

    Feeling Stuck in Life? Discover How You Can Unlock Your True Potential

    • By Milton
    • January 11, 2026
    • 13 views
    Feeling Stuck in Life? Discover How You Can Unlock Your True Potential

    BREAKING: Algeria Is Set To File Complaints To CAF About What They Call Bad Refereeing In Their AFCON Quarterfinal Loss To Nigeria

    • By Milton
    • January 11, 2026
    • 21 views
    BREAKING: Algeria Is Set To File Complaints To CAF About What They Call Bad Refereeing In Their AFCON Quarterfinal Loss To Nigeria

    Every Relationship I Entered Ended in Pain Until I Finally Found the Real Cause

    • By Milton
    • January 10, 2026
    • 20 views
    Every Relationship I Entered Ended in Pain Until I Finally Found the Real Cause

    I Was Always Sick No Matter How Much Medicine I Took, Until My Health Was Restored

    • By Milton
    • January 10, 2026
    • 17 views
    I Was Always Sick No Matter How Much Medicine I Took, Until My Health Was Restored