Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  Sad Photo Of The Day

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  7 Things To Do When You're Broke

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    Today 16th April 2026 || Newspaper Headlines

    Today 16th April 2026 || Newspaper Headlines 📰 Taifa Leo — “Ni Kubaya”📰 Daily Nation — “Pumping up pain”📰 People Daily — “Inside the Judiciary crisis”📰 The Standard — “Double-speak…

    Read more

    • MiltonMilton
    • News
    • April 16, 2026
    • 3 views
    • 2 minutes Read
    The Silent Story Behind The Viral “Kwa Mbae” Boy

    The silent story behind the viral “Kwa Mbae” boy. Stepping into Ituntu Village, one might easily overlook this modest homestead. But behind its quiet appearance lies a powerful story that…

    Read more

    You Missed

    Today 16th April 2026 || Newspaper Headlines

    • By Milton
    • April 16, 2026
    • 2 views
    Today 16th April 2026 || Newspaper Headlines

    The Silent Story Behind The Viral “Kwa Mbae” Boy

    • By Milton
    • April 16, 2026
    • 3 views
    The Silent Story Behind The Viral “Kwa Mbae” Boy

    Wednesday’s Football Results

    • By Milton
    • April 16, 2026
    • 3 views
    Wednesday’s Football Results

    What Energy CS Opiyo Said About Fuel Prices Increase

    • By Milton
    • April 15, 2026
    • 6 views
    What Energy CS Opiyo Said About Fuel Prices Increase

    Update: Opposition Leaders Speaks About Fuel Prices

    • By Milton
    • April 15, 2026
    • 7 views
    Update: Opposition Leaders Speaks About Fuel Prices

    Fuel Is High. Let Me Give You A Quick Review Of What Is Going To Happen

    • By Milton
    • April 15, 2026
    • 7 views
    Fuel Is High. Let Me Give You A Quick Review Of What Is Going To Happen