Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  How To Produce Maggot

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  Gor Mahia Chairman Ambrose Rachier Accused Nairobi United Fans For Chaos

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    Football Titbits across the papers

    Football Titbits across the papers. Liverpool make offer for Dutch defender Sam Beukema, AC Milan offer Rafael Leao to Premier League sides, Manchester United target ex-Nottingham Forest midfielder Danilo. Liverpool…

    Read more

    • MiltonMilton
    • News
    • April 30, 2026
    • 8 views
    • 1 minute Read
    UPDATE: President Ruto Awards Sebastian Sawe With Ksh 8 Million

    President Ruto awards Sebastian Sawe with Ksh 8 Million after becoming the first athlete to run a sub-two-hour marathon at the 2026 London Marathon. READ Also  Boni Khalwale Reveals Raila’s…

    Read more

    You Missed

    Football Titbits across the papers

    • By Milton
    • May 3, 2026
    • 3 views
    Football Titbits across the papers

    UPDATE: President Ruto Awards Sebastian Sawe With Ksh 8 Million

    • By Milton
    • April 30, 2026
    • 8 views
    UPDATE: President Ruto Awards Sebastian Sawe With Ksh 8 Million

    UPDATE: Millie Odhiambo Rejects Election Zoning

    • By Milton
    • April 30, 2026
    • 7 views
    UPDATE: Millie Odhiambo Rejects Election Zoning

    Football Titbits across the papers

    • By Milton
    • April 30, 2026
    • 7 views
    Football Titbits across the papers

    I Still Believe Arsenal Will Win The Premier League

    • By Milton
    • April 20, 2026
    • 20 views
    I Still Believe Arsenal Will Win The Premier League

    Pep Guardiola On Donnarumma’s error

    • By Milton
    • April 20, 2026
    • 20 views
    Pep Guardiola On Donnarumma’s error