Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  “My Wife Whom I Share 3 Children With Dumped Me For A Younger Man But This Made Her Return Immediately” Patrick Tells

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  Riggy G’s Specialist Bodyguard Is A Force Of Nature Wrapped In Muscle And Menace

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    • MiltonMilton
    • News
    • December 7, 2025
    • 2 views
    • 2 minutes Read
    DCI Nab 26 Suspects In Illegal Issuance Of Vital Government Documents

    In a meticulously coordinated operation, detectives have arrested 26 individuals implicated in the unlawful and unprocedural acquisition of vital government documents, including National Identity Cards, Passports, Birth Certificates, and Foreigner/Alien…

    Read more

    • MiltonMilton
    • News
    • December 7, 2025
    • 3 views
    • 1 minute Read
    5 Arrested In Mulot Digital Fraud Crackdown

    In a swift response to mobile banking fraud in Mulot, detectives launched a coordinated operation that resulted in the arrest of five suspects at the bustling Mulot market. The suspects,…

    Read more

    You Missed

    DCI Nab 26 Suspects In Illegal Issuance Of Vital Government Documents

    • By Milton
    • December 7, 2025
    • 2 views
    DCI Nab 26 Suspects In Illegal Issuance Of Vital Government Documents

    5 Arrested In Mulot Digital Fraud Crackdown

    • By Milton
    • December 7, 2025
    • 3 views
    5 Arrested In Mulot Digital Fraud Crackdown

    Receiving Day-Old Chicks (DAY 1–6)

    • By Milton
    • December 6, 2025
    • 3 views
    Receiving Day-Old Chicks (DAY 1–6)

    Today’s Premier League Matches

    • By Milton
    • December 6, 2025
    • 5 views
    Today’s Premier League Matches

    Eulogy For Beryl Odinga By Paul Ambala, Grandson Of Otieno Ambala

    • By Milton
    • December 6, 2025
    • 5 views
    Eulogy For Beryl Odinga By Paul Ambala, Grandson Of Otieno Ambala

    Update: Nyamira Governor Still In Trouble Despite Senate’s Decision

    • By Milton
    • December 6, 2025
    • 5 views
    Update: Nyamira Governor Still In Trouble Despite Senate’s Decision