Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  Crazy World! A Tanzanian man lived with a knife in his chest for 8 years

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  Can you stay awake from 1 AM to 5 AM?

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    Today’s Newspaper: Kindiki Stripped

    Breaking news Kindiki has been removed from the crucial role he previously held of coordinating government operations across all ministries — the Intergovernmental Coordination function. This responsibility has now been…

    Read more

    CR7 Us Reportedly Set To Retire

    CR7 is reportedly set to retire from international football after Portugal’s UEFA Nations League clash against Wales on Sep 24. Portugal career: READ Also  Netanyahu Said: “World Hates Israel for…

    Read more

    You Missed

    Today’s Newspaper: Kindiki Stripped

    • By Milton
    • July 28, 2026
    • 7 views
    Today’s Newspaper: Kindiki Stripped

    CR7 Us Reportedly Set To Retire

    • By Milton
    • July 25, 2026
    • 5 views
    CR7 Us Reportedly Set To Retire

    Update: Iran Expands Conflict Through Regional Proxy

    • By Milton
    • July 25, 2026
    • 11 views
    Update: Iran Expands Conflict Through Regional Proxy

    Lamine Yamal Has Never Lost To Kylian Mbappe In A Knockout Match

    • By Milton
    • July 14, 2026
    • 15 views
    Lamine Yamal Has Never Lost To Kylian Mbappe In A Knockout Match

    U.S. Naval Blockade On Iran Takes Effect

    • By Milton
    • July 14, 2026
    • 17 views
    U.S. Naval Blockade On Iran Takes Effect

    A Man Drove The Same Car For 15 Years Trying To Reach 1,000,000 Kilometres

    • By Milton
    • July 14, 2026
    • 19 views
    A Man Drove The Same Car For 15 Years Trying To Reach 1,000,000 Kilometres