Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  CAF Champions League Group C Fixtures

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  How To Heal From Broken Marriages Caused By Negative Energies

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    Today’s EPL Fixture

    SUNDAY 6th SEPTEMBER 2026 EPL FIXTURES Everton Vs Manchester United 4 PM MATCH OF THE DAY Arsenal Vs Chelsea Venue :Emirates Stadium Time: 6:30 PM MATCH FACTS Gunners Arsenal are…

    Read more

    𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: Iran Fires Missiles at U.S. Warships, U.S. Strikes Three Iranian Oil Tankers

    Iran’s Islamic Revolutionary Guard Corps (IRGC) launched ballistic missiles toward two U.S. Navy warships, including a U.S. aircraft carrier and a guided-missile destroyer, in regional waters. U.S. Central Command (CENTCOM)…

    Read more

    You Missed

    Today’s EPL Fixture

    • By Milton
    • September 6, 2026
    • 2 views
    Today’s EPL Fixture

    𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: Iran Fires Missiles at U.S. Warships, U.S. Strikes Three Iranian Oil Tankers

    • By Milton
    • September 6, 2026
    • 4 views
    𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: Iran Fires Missiles at U.S. Warships, U.S. Strikes Three Iranian Oil Tankers

    Football Titbits Across The Papers

    • By Milton
    • September 6, 2026
    • 4 views
    Football Titbits Across The Papers

    𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: U.S. Sanctions Turkish Bank Over Alleged Iran Financial Network

    • By Milton
    • September 5, 2026
    • 5 views
    𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: U.S. Sanctions Turkish Bank Over Alleged Iran Financial Network

    𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: Large Explosion at Military Barracks in Bolivia Kills at Least 10

    • By Milton
    • September 5, 2026
    • 6 views
    𝗕𝗥𝗘𝗔𝗞𝗜𝗡𝗚: Large Explosion at Military Barracks in Bolivia Kills at Least 10

    Football Titbits Across The Papers

    • By Milton
    • September 5, 2026
    • 4 views
    Football Titbits Across The Papers