Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  Update: President Ruto Nominates Ida Odinga As Kenya's Ambassador

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  My Own Husband Cheated On Me With My Cousin Sister & Dumped Me, Congo Woman Cries

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    Lamine Yamal Has Never Lost To Kylian Mbappe In A Knockout Match

    Lamine Yamal has 𝐍𝐄𝐕𝐄𝐑 𝐋𝐎𝐒𝐓 to Kylian Mbappé in a knockout match. ✅ EURO semi-final – 2024✅ Supercopa final – 2025✅ Copa del Rey final – 2025✅ Nations League semi-final…

    Read more

    U.S. Naval Blockade On Iran Takes Effect

    The U.S. naval blockade targeting Iranian ports and oil facilities has officially entered into force, according to previous announcements by U.S. Central Command (CENTCOM). U.S. and allied naval forces have…

    Read more

    You Missed

    Lamine Yamal Has Never Lost To Kylian Mbappe In A Knockout Match

    • By Milton
    • July 14, 2026
    • 8 views
    Lamine Yamal Has Never Lost To Kylian Mbappe In A Knockout Match

    U.S. Naval Blockade On Iran Takes Effect

    • By Milton
    • July 14, 2026
    • 9 views
    U.S. Naval Blockade On Iran Takes Effect

    A Man Drove The Same Car For 15 Years Trying To Reach 1,000,000 Kilometres

    • By Milton
    • July 14, 2026
    • 10 views
    A Man Drove The Same Car For 15 Years Trying To Reach 1,000,000 Kilometres

    A Tanker Was Struck By A Missile Off The Coast Of Oman

    • By Milton
    • July 14, 2026
    • 12 views
    A Tanker Was Struck By A Missile Off The Coast Of Oman

    Why Since 2018, Kylian Mbappe’s Hasn’t Touched A Single Salary

    • By Milton
    • July 14, 2026
    • 13 views
    Why Since 2018, Kylian Mbappe’s Hasn’t Touched A Single Salary

    Details Of France Vs Spain Semifinal

    • By Milton
    • July 14, 2026
    • 11 views
    Details Of France Vs Spain Semifinal