Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  Jay Jay Okocha, Nigeria football legend, on Nigeria’s World Cup qualification

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  "Teaching kids maths is not your job," said comedian Mammito Eunice

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    Update: Ndindi Nyoro Wins Big

    Glad to have received great leaders joining the People’s Party today. We received; Hon Esther Irungu – MCA, Kiambu County. Hon Anthony Marubu (Manucho) – Currently MCA in Murang’a. Both…

    Read more

    • MiltonMilton
    • News
    • August 18, 2026
    • 2 views
    • 2 minutes Read
    Update: Okoth Obado In Court Again

    Convicted former Migori Governor Okoth Obado and his co-convicts are set to return to the Milimani High Court today for a virtual mention in the highly scrutinised Sharon Otieno murder…

    Read more

    You Missed

    Update: Ndindi Nyoro Wins Big

    • By Milton
    • August 18, 2026
    • 2 views
    Update: Ndindi Nyoro Wins Big

    Update: Okoth Obado In Court Again

    • By Milton
    • August 18, 2026
    • 2 views
    Update: Okoth Obado In Court Again

    WAFCON 2026 AWARD WINNERS

    • By Milton
    • August 18, 2026
    • 3 views
    WAFCON 2026 AWARD WINNERS

    Weather Forecast For 18th to 24th August 2026

    • By Milton
    • August 18, 2026
    • 6 views
    Weather Forecast For 18th to 24th August 2026

    Opinion: Ruto’s Top Leaders Who Will Ditch Him

    • By Milton
    • August 18, 2026
    • 8 views
    Opinion: Ruto’s Top Leaders Who Will Ditch Him

    𝗔𝗡𝗔𝗟𝗬𝗦𝗜𝗦: Iran Uses Low-Cost Drones to Pressure U.S. Air Defenses

    • By Milton
    • August 15, 2026
    • 13 views
    𝗔𝗡𝗔𝗟𝗬𝗦𝗜𝗦: Iran Uses Low-Cost Drones to Pressure U.S. Air Defenses