Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  Here Is The Total Number Of New Registered Voters

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  “I Nabbed My Husband Cheating On Me With My Cousin Sister, It Pained Me Alot” Beatrice Akello Tells

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    Gaddafi’s Son Saif al-Islam Killed In Deadly Attack At Zintan Home

    Gaddafi’s son Saif al-Islam killed in deadly attack at Zintan homeHis French lawyer, Marcel Ceccaldi, told AFP that Saif al-Islam, 53, was killed on Tuesday afternoon after gunmen stormed his…

    Read more

    Wembley Awaits: 𝐀𝐫𝐬𝐞𝐧𝐚𝐥 vs 𝐌𝐚𝐧𝐜𝐡𝐞𝐬𝐭𝐞𝐫 𝐂𝐢𝐭𝐲

    𝐖𝐄𝐌𝐁𝐋𝐄𝐘 𝐀𝐖𝐀𝐈𝐓𝐒. 𝐀𝐫𝐬𝐞𝐧𝐚𝐥 vs 𝐌𝐚𝐧𝐜𝐡𝐞𝐬𝐭𝐞𝐫 𝐂𝐢𝐭𝐲.Under the arch. On the grandest domestic stage. City dismantled Newcastle.Arsenal stormed past Chelsea. Now… the collision is set. 𝐀𝐫𝐭𝐞𝐭𝐚 vs 𝐆𝐮𝐚𝐫𝐝𝐢𝐨𝐥𝐚Student vs master.Ideas vs…

    Read more

    You Missed

    Gaddafi’s Son Saif al-Islam Killed In Deadly Attack At Zintan Home

    • By Milton
    • February 5, 2026
    • 13 views
    Gaddafi’s Son Saif al-Islam Killed In Deadly Attack At Zintan Home

    Wembley Awaits: 𝐀𝐫𝐬𝐞𝐧𝐚𝐥 vs 𝐌𝐚𝐧𝐜𝐡𝐞𝐬𝐭𝐞𝐫 𝐂𝐢𝐭𝐲

    • By Milton
    • February 5, 2026
    • 6 views
    Wembley Awaits: 𝐀𝐫𝐬𝐞𝐧𝐚𝐥 vs 𝐌𝐚𝐧𝐜𝐡𝐞𝐬𝐭𝐞𝐫 𝐂𝐢𝐭𝐲

    Wife Of The layte Saif al-Islam Gaddafi, Gaddafi’s Recently Murdered Son Shares His Final Words

    • By Milton
    • February 5, 2026
    • 13 views
    Wife Of The layte Saif al-Islam Gaddafi, Gaddafi’s Recently Murdered Son Shares His Final Words

    Testing the Red Line? Iran Probes U.S. Navy Twice in Hours Ahead Of Oman Talks

    • By Milton
    • February 4, 2026
    • 17 views
    Testing the Red Line? Iran Probes U.S. Navy Twice in Hours Ahead Of Oman Talks

    𝗠𝘂𝗵𝗼𝗼𝘇𝗶 𝗛𝗶𝗻𝘁𝘀 𝗨𝗻𝗰𝗹𝗲 𝗦𝗮𝗹𝗶𝗺 𝗦𝗮𝗹𝗲𝗵 𝗖𝗼𝘂𝗹𝗱 𝗦𝘂𝗰𝗰𝗲𝗲𝗱 𝗠𝘂𝘀𝗲𝘃𝗲𝗻𝗶!

    • By Milton
    • February 4, 2026
    • 10 views
    𝗠𝘂𝗵𝗼𝗼𝘇𝗶 𝗛𝗶𝗻𝘁𝘀 𝗨𝗻𝗰𝗹𝗲 𝗦𝗮𝗹𝗶𝗺 𝗦𝗮𝗹𝗲𝗵 𝗖𝗼𝘂𝗹𝗱 𝗦𝘂𝗰𝗰𝗲𝗲𝗱 𝗠𝘂𝘀𝗲𝘃𝗲𝗻𝗶!

    What Would Happen If The United States Strikes Iran?

    • By Milton
    • February 4, 2026
    • 35 views
    What Would Happen If The United States Strikes Iran?