Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  Gachagua Is Considering Fronting Babu Owino As His Candidate From Nairobi Governor

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  Politics In Kenya Is Never Boring, And This Week, The Tea Is Piping Hot

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    “I almost died in January, the window between life and death for me was 12 hours.”

    Renowned radio presenter Kamene Goro has opened up after months away from the public eye, revealing she was battling a disease that nearly took her life. “I almost died in…

    Read more

    I’m Getting Briefings That Cleo Malalah Is Considering A Move To ODM

    I’m getting briefings that Cleo Malalah is considering a move to ODM to vie for the Kakamega Senatorial seat and could formally join at tomorrow’s ODM NDC in Nairobi Reports…

    Read more

    You Missed

    “I almost died in January, the window between life and death for me was 12 hours.”

    • By Milton
    • March 28, 2026
    • 1 views
    “I almost died in January, the window between life and death for me was 12 hours.”

    I’m Getting Briefings That Cleo Malalah Is Considering A Move To ODM

    • By Milton
    • March 27, 2026
    • 2 views
    I’m Getting Briefings That Cleo Malalah Is Considering A Move To ODM

    Update: Australia Imposes Temporary Entry Ban On Iranian Passport Holders

    • By Milton
    • March 26, 2026
    • 4 views
    Update: Australia Imposes Temporary Entry Ban On Iranian Passport Holders

    Ongoing construction of the Kiandutu Modern Market in the Kiandutu area, Thika Township Ward, Thika Constituency.

    • By Milton
    • March 26, 2026
    • 6 views
    Ongoing construction of the Kiandutu Modern Market in the Kiandutu area, Thika Township Ward, Thika Constituency.

    Update: EU and Australia reach landmark trade deal after 8 years of negotiations

    • By Milton
    • March 26, 2026
    • 8 views
    Update: EU and Australia reach landmark trade deal after 8 years of negotiations

    Update: Iran sets sweeping ceasefire terms, demands major U.S. and Israeli concessions

    • By Milton
    • March 26, 2026
    • 13 views
    Update: Iran sets sweeping ceasefire terms, demands major U.S. and Israeli concessions