Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló Apinduliwa

Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló amepinduliwa. Rais Umaro ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa kijeshi baada ya milio ya risasi kusikika katika mji mkuu, Bissau kwa siku 3 mfululizo. Shirika la habari la BBC limeripoti kwamba Rais huyo ametiwa mbaroni na maafisa wa kijeshi na kwa sasa yupo chini ya ulinzi.

Brigedia Jenerali Denis N’Canha, mkuu wa Brigedi ya kijeshi mjini Bisau amehutubia kupitia televisheni ya taifa na kutangaza kuwa jeshi limechukua madaraka. Jenerali N’Canha amesema askari wote wa kikosi cha ulinzi cha Rais wamekamatwa pamoja na mawaziri kadhaa.

Kabla ya Jeshi kutangaza mapinduzi hayo, Rais Sissoco alipiga simu kwenye kituo cha televisheni cha France 24 kilichopo Ufaransa kwa sauti ya kutetemeka na kusema: “Nimewekwa chini ya ulinzi, nimeondolewa madarakani” kabla ya simu hiyo kukatwa ghafla.

READ Also  From Suffering In Saudi Arabia To Heroic Welcome In Mugondoi Village

Guinea-Bissau ilikuwa ikisubiri matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili, ambapo mgombea mkuu wa upinzani Fernando Dias alienguliwa katika orodha ya wagombea ili kumfanya Rais Umaro ashinde kirahisi.

Jenerali N’Canha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya awali ya uchaguzi yaliyoonyesha kumpa ushindi Rais Umaro kwa zaidi ya 90% na amesema uchaguzi huo ulijaa udanganyifu mkubwa. Jenerali N’Canha ametangaza kufunga mipaka ya nchi, huku akiwataka wananchi wabaki watulivu. Pia ameeleza kuwa Jeshi litaongoza nchi hiyo kwa muda mfupi ili kurejesha hali ya utulivu kabla ya kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Rais Umaro alikuwa Rais wa kwanza Afrika kumpongeza Rais Samia baada ya matokeo ya uchaguzi wa Tanzania kutangazwa. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Rais Umaro alipost picha akiwa na Rais Samia na kuandika maneno yafuatayo: “Napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia Suluhu kwa kuchaguliwa tena. Ushindi huu ni ushahidi wa imani ambayo wananchi wa Tanzania wamempa na ni kielelezo cha dhamira yake thabiti ya kuendeleza na kustawisha Tanzania.”

READ Also  Update: KCSE Results To Be Announced On This Day

Nini maoni yako??

  • Milton

    Professional IT expert and experienced news writer/ online marketing expert

    Related Posts

    BREAKING: Algeria Is Set To File Complaints To CAF About What They Call Bad Refereeing In Their AFCON Quarterfinal Loss To Nigeria

    The Algerian FA states: ■ They were denied a clear penalty. ■ Many calls by Senegalese referee Issa Sy were questionable. ■ The referee seemed to favor Nigeria. ■ Issa…

    Read more

    • MiltonMilton
    • News
    • January 10, 2026
    • 18 views
    • 4 minutes Read
    Every Relationship I Entered Ended in Pain Until I Finally Found the Real Cause

    Sarah, a 33-year-old woman from Nyeri County, Kenya, had always believed in love. She entered relationships with hope, commitment, and genuine intentions. At the beginning, everything would feel perfect. Her…

    Read more

    You Missed

    BREAKING: Algeria Is Set To File Complaints To CAF About What They Call Bad Refereeing In Their AFCON Quarterfinal Loss To Nigeria

    • By Milton
    • January 11, 2026
    • 16 views
    BREAKING: Algeria Is Set To File Complaints To CAF About What They Call Bad Refereeing In Their AFCON Quarterfinal Loss To Nigeria

    Every Relationship I Entered Ended in Pain Until I Finally Found the Real Cause

    • By Milton
    • January 10, 2026
    • 18 views
    Every Relationship I Entered Ended in Pain Until I Finally Found the Real Cause

    I Was Always Sick No Matter How Much Medicine I Took, Until My Health Was Restored

    • By Milton
    • January 10, 2026
    • 15 views
    I Was Always Sick No Matter How Much Medicine I Took, Until My Health Was Restored

    UPDATE: President William Ruto Has Reappointed Reverend Dr Stephen Mairori

    • By Milton
    • January 10, 2026
    • 22 views
    UPDATE: President William Ruto Has Reappointed Reverend Dr Stephen Mairori

    Kenya Premier League Fixtures

    • By Milton
    • January 10, 2026
    • 15 views
    Kenya Premier League Fixtures

    My Children Failed in School No Matter How Hard They Tried, Until Things Changed Suddenly

    • By Milton
    • January 10, 2026
    • 20 views
    My Children Failed in School No Matter How Hard They Tried, Until Things Changed Suddenly